Serikali ya Ethiopia imekiri kuchukua hatua za kuzuia kituo cha radio cha Marekani, VOA, Kupeperusha matangazo yake nchini humo mbali na kubana matangazo yake.
Mahakama ya Kimataifa ya ICTR, imetupilia mbali rufaa iliyowasilishwa mbele yake dhidi ya hukumu ya kifungo cha miaka 15 iliyoitoa awali kwa mwimbaji Simon Bikindi.
Hatimaye timu zitakazopambana hatua ya robo fainali kuwania ubingwa wa vilabu vya Ulaya maarufu Champions League zimejulikana, huku Arsenal wakianza na Barcelona wakati Manchester United wataanzia ugenini Ujerumani wakichuana na Bayern Munich.
Kocha wa England Fabio Capello amemualika David Beckham kujiunga na kikosi cha England cha Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini licha ya kiungo huyo kuwa ameumia.
Idhaa ya Kiswahili ya BBC inafanya vipindi mbali mbali vya kukumbuka miaka 20 tangu kifo cha hayati Luambo Makiadi, a.k.a Franco, mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
BBC World News, katika mfululizo wa vipindi maalum vya televisheni na radio, vile vile online, wameanzisha shindano la kuandaa makala fupi ya video - iwe ni umeipiga kwa digital camera au mobile phone camera, ruksa!