Michael Schumacher , dereva wa mashindano ya magari mwenye mafanikio zaidi katika historia anatarajiwa kurejea kuendeshea timu ya Mercedes, kwa mujibu wa Eddie Jordan mchambuzi wa F1 katika BBC.
Kuna mjadala iwapo mechi kati ya Ireland na Ufaransa irudiwe au la. Mshambulizi Thierry Henry ambaye ujanja wake umesababisha hamasa anaomba mechi irudiwe nayo FIFA ikisema ng'o!
Idhaa ya Kiswahili ya BBC inafanya vipindi mbali mbali vya kukumbuka miaka 20 tangu kifo cha hayati Luambo Makiadi, a.k.a Franco, mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Lilikuwa pambano la kipekee, ambalo bara la Afrika halijabahatika kushuhudia kwa miaka 35 iliyopita. Mwezi Oktoba, imetimia miaka 35 tangu Mohammed Ali atwangane na George Foreman, jijini Kinshasa.
Baada ya ukame wa muda mrefu, mvua kubwa zilipoanza kunyesha katika mkoa wa Kaskazini Mashariki nchini Kenya zilisababisha mafuriko yaliyobomoa miundo mbinu kama barabara.