Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu, amesema ataharakisha kesi za watuhumiwa waliochechea vurugu baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka 2007.
Shirika la misaada la madaktari wasio na mipaka MSF, limedai jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, lilitumia kliniki za chanjo kama chambo kuwashambulia raia.
Timu ya vijana wenye umri ulio chini ya miaka kumi na saba inasherehekea kufuzu kwa robo fainali ya Kombe la Dunia la vijana wenye umri huo nchini Nigeria.
Afisa mmoja mkuu wa riadha nchini Afrika kusini ameachishwa kazi kwa muda kuhusiana na namna alivyoshughulikia kashfa kuhusu jinsia ya mwanariadha Caster Semenya.
Lilikuwa pambano la kipekee, ambalo bara la Afrika halijabahatika kushuhudia kwa miaka 35 iliyopita. Mwezi Oktoba, imetimia miaka 35 tangu Mohammed Ali atwangane na George Foreman, jijini Kinshasa.