Watu 22 wamehukumiwa kifungo cha miaka sita na mahakama moja katika jimbo la Puntland, nchini Somalia, kwa kupatikana na hatia ya kuhusika na uharamia.
Kamati ya bunge ya Kenya inayojadili vipengele vya katiba mpya iliyosubiriwa kwa muda mrefu imependekeza nusu ya wajumbe wa baraza jipya la senate litakalokuwa na uwezo mkubwa wawe wanawake.
Barua kutoka kwa Papa Benedict akijibu kwa mara ya kwanza hadharini kuhusu unyanyasaji wa kimapenzi na kuwatendea vibaya watoto uliofanywa na maaskofu nchini Ireland itachapishwa hivi karibuni.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ameanza ziara Mashariki ya Kati kujaribu kuzishawishi Israel na Palestina waanzishe upya mazungumzo ya amani yaliyokwama.
Timu inayojitahidi ishushe daraja ya Wolves imeshindwa kusogea juu zaidi baada ya John Carew kuisawzishia Aston Villa dakika za mwisho na timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2.
Shirikisho la Soka la Algeria (Faf) limeshindwa rufaa yake ya Kombe la Dunia inayohusiana na kutenguliwa adhabu ya kufungiwa Nadir Belhadj na Faouzi Chaouchi.
Mlinda mlango wa Manchester City Shay Given amesema wanakabiliwa na chagizo kumaliza Ligi Kuu ya England nafasi ya nne ili kuweza kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu ujao.
Idhaa ya Kiswahili ya BBC inafanya vipindi mbali mbali vya kukumbuka miaka 20 tangu kifo cha hayati Luambo Makiadi, a.k.a Franco, mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
BBC World News, katika mfululizo wa vipindi maalum vya televisheni na radio, vile vile online, wameanzisha shindano la kuandaa makala fupi ya video - iwe ni umeipiga kwa digital camera au mobile phone camera, ruksa!